Mwanaume moja wa miaka 38 ameponea kifo baada ya jaribio la kujitoa uhai kwa kujinyonga kutibuka usiku wa kuamkia leo katika kijiji cha Soweto mjini Laisamis kaunti ya Marsabit.
February 7, 2025
Na Caroline Waforo
Wakaazi kaunti ya Marsabit wametahadharishwa dhidi ya kutuma maombi ya kupata vitambulisho zaidi ya moja.
Akizungumza na Shajara afisini mwake afisa wa usajili jimboni Marsabit Michael Oduor amesema kuwa hili litahitilafiana na shughuli za kuchapisha vitambulisho.
Hii ni kutokana na malalamishi ya kucheleweshwa kwa vitambulisho kutoka kwa baadhi ya wakaazi ambapo anasema kuwa mara kwa mara wakaazi wanaamua kutuma maombi tena.
Itakumbukwa kuwa vinavyochapishwa ni vitambulisho vya kidigitali maisha card.
Afisi ya usajili Marsabit imetuma maombi ya vitambulisho hivyo takriban 18,973.
Aidha Vitambulisho vya kidigatli 12,590 vimechapishwa na kutumwa jimboni huku 12,388 tayari vikiwa vimechukuliwa.