Local Bulletins

VIJANA WAWILI WAJERUHIWA KWA RISASI NA WATU WASIOJULIKANA ENEO LA KARANTINA, SAKU KAUNTI YA MARSABIT.

Na Talaso Huka

Vijana wawili wamejeruhiwa usiku wa kuamkia leo baada ya kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana. Tukio hilo lilitokea eneo la Karantina, Saku kaunti ya Marsabit.

Akidhibitisha kisa hicho kamanda wa polisi kaunti ya Marsabit Leonard Kimaiyo amesema kuwa uchunguzi unaendelea huku akibainisha kuwa lengo la mavamizi hayo hayajulikani.

Hata hivyo amesema kuwa vijana hao wanaendelea kupata matibabu katika hospitali ya rufaa ya Marsabit.

Subscribe to eNewsletter