Local Bulletins

SHULE 38 ZA UPILI KATIKA KAUNTI YA MARSABIT ZANUFAIKA NA MSAADA WA CHAKULA KUTOKA KWA SEREKALI YA KITAIFA..

Na Isaac Waihenya,

Shule 38 za upili katika kaunti ya Marsabit zimenenufaika na msaada kutoka kwa serekali ya kitaifa ambao unalenga kuwalipia karo watoto kutoka familia maskini.

Kwa mujibu wa katibu wa kudumu katika idara ya maeneo kama na maendeleo ya mikoa Kello Harama ni kuwa shule 13 katika eneo bunge la Saku zimenufaika, Moyale shule 5 huku shule 8 katika maeneo bunge ya North Horr na Laisamis zikinufaika katika mradi huo unaolenga kuzipa shule chakula kwa niamba ya karo.

Akizungumza alipokutana na walimu wakuu wa shule zinazonufaika na mradi huyo Kello ametaja kwamba serekali ianlenga kuhakikisha kuwa wanafunzi kutoka maeneo kame wanapokea elimu bila kutatizika sawa na wenzao waliokatika maeneo mengini.

Kadhalika Kello ameahidi kuwa dara yake itaendeleza zoezi la kuchimba mabwawa katika maneo mbalimbali hapa jimboni ili kutatua zoezi la ukosefu wa maji.

Subscribe to eNewsletter