Local Bulletins

RAIA WAWILI WA KIGENI WAMEFIKISHWA KATIKA MAHAKAMA YA MARSABIT KWA KOSA LA KUWA NCHINI BILA STAKABADHI ZOZOTE.

Na Grace Gumato

Raia wawili wa kigeni wamefikishwa katika mahakama ya Marsabit kwa kosa la kuwa nchini bila stakabadhi zozote.

Wa kwanza ni mwanaume mmoja mwenye umri wa makamu ambaye ni raia wa Ethiopia aliyefikishwa mahakammni kwa kosa la kuingia Kenya bila kuwa na shtaka badhi yoyote ya kumruhusu kuwa nchini.

Mshukiwa Mamushi Bancha Olongo anadaiwa kuwa mnamo terehe 19 mwezi  mwaka huu eneo la Karantina  katika kaunti ya Marsabit alipatika katika taifa hii bila kuwa na stakabadhi yoyote.

Mshukiwa alifikishwa mbele ya hakimu mkaazi Simon Arome na kukubali mshataka dhidi yake huku mahakama ikimpa kifungo cha miezi 9 ama faini ya shilling 50,000.

Mshukiwa wa pili amekuwa Devisi Ahibisimwe aliyefikishwa katika mahakama ya Marsabit kwa kosa la kupatikana nchini bila kuwa na stakabdhi yoyote.

Mshukiwa ambaye ni raia wa Uganda anadiwa kuwa mnamo tarehe 17 mwezi wa Mei mwaka huu katika maeneo ya Loyangalani alipatika katika taifa la Kenya bila kuwa na stakabdhi yoyote pia.

Mshukiwa alifikishwa mbele ya hakimu mkaazi Simon Arome na kukubali mshtaka dhidi yake huku mahakama ikiamuru mshukiwa kupelekwa katika ubalozi wa Uganda ili kurudishwa katika taifa la Uganda.

Subscribe to eNewsletter