Local Bulletins

MWANAUME MOJA AMESHTAKIWA KATIKA MAHAKAMA YA MARSABIT KWA KOSA LA WIZI WA MIFUGO TAKRIBAN 213.

NA CAROL WAFORO

Mwanaume moja ameshtakiwa katika mahakama ya marsabit kwa kosa la wizi wa mifugo takriban 213.

Inadaiwa kuwa mnamo tarehe 18 Juni mwaka 2024 katika lokesheni ya badassa kaunti ndogo ya Marsabit ya kati, kwa ushirikiano na watu wengine waliojihamu kwa bunduki mshukiwa George Leado almaarufu Lemurdato walitekeleza wizi wa ngombe takriban 213 wenye dhamana ya shilingi milioni 13,845,000 mali yake Boru Jarso.

Leado alikamatwa tarehe 21/6/2024 na kufikishwa mahakamani Jumatatu ya tarehe 29/7/2024 mbele ya hakimu SK Arome ambapo alikana mashtaka dhdi yake.

Mshukiwa anauguza majeraha na hivyo mahakama iliagiza azuiliwa katika jela ya Meru ili kumwezesha kupata matibabu katika hospitali ya rufaa ya Meru.

Kesi hiyo itatajwa tena tarehe 13 mwezi Agosti 2024.

Subscribe to eNewsletter