Mwanaume moja wa miaka 38 ameponea kifo baada ya jaribio la kujitoa uhai kwa kujinyonga kutibuka usiku wa kuamkia leo katika kijiji cha Soweto mjini Laisamis kaunti ya Marsabit.
February 7, 2025
Na Samuel Kosgei
Mbunge wa Laisamis Joseph Lekuton amependekeza bunge kubuni kutengeneza sheria itakayoruhusu wakenya wanaoaga dunia kupeana viungo vya mwili kwa hiari akisema hatua hiyo itasaidia wakenya wanaohitaji viungo hivyo.
Lekuton akizungumza kwenye hafla ya kutoa damu katika hospitali kuu ya Marsabit Ijumaa amesema – kama vile wakenya husaidia wakenya wenzao kuwapa damu ili kunusuru maisha itakuwa jambo la busara pia kukubali kupeana viungo muhumu vya mwili mtu anapofariki kama vile martaifa ya kigeni hufanya.