Local Bulletins

MARSABIT YAADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUPANDA MICHE 150 YA MITI

NA CAROLINE WAFORO

Katika sherehe za maadhimisho zilizofanyika katika Shule ya Msingi ya Marsabit Full Primary, Naibu Msimamizi wa Misitu KFS Kadiro Oche alisema kuwa idadi ndogo ya miche 150 iliyopandwa inatokana na upungufu wa mvua.

Kadhalika, Oche alitoa wito kwa wakazi pamoja na wadau wengine katika Kaunti ya Marsabit kushiriki katika shughuli za utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti ili kutimiza lengo la serikali la kupanda miti bilioni 15 ifikapo mwaka 2030.

Akizungumza katika hafla hiyo, Msaidizi wa Kamishna wa Kaunti Festus Chepkwonyi, aliyezungumza kwa niaba ya Kamishna wa Kaunti, ametoa changamoto kwa Manispaa ya Mji wa Marsabit kuhakikisha kuwa hakuna mirundiko ya takataka.

Imekumbukwa kuwa kumekuwepo na ongezeko la takataka katika kaunti, hasa katika mji wa Marsabit na Moyale.

Subscribe to eNewsletter