Mwanaume moja wa miaka 38 ameponea kifo baada ya jaribio la kujitoa uhai kwa kujinyonga kutibuka usiku wa kuamkia leo katika kijiji cha Soweto mjini Laisamis kaunti ya Marsabit.
February 7, 2025
Na Carol Waforo
Mapambano makali kati ya maafisa wa polisi na wahalifu wa wizi wa mifugo yalifanyika mapema Jumatatu katikati ya barabara ya HulaHula kuelekea Kargi kaunti ya Marsabit.
Kulingana na Kaimu Kamishna wa kaunti ya Marsabit David Saruni kundi la wezi wa mifugo lilishambulia gari moja la uchukuzi lililokuwa likielekea Moyale usiku wa kuamkia leo
Anasema kuwa wahalifu hao walikuwa na nia ya kuiba mifugo ila hawakufanikiwa na ndiposa wakaamua kushambulia gari la uchukuzi barabarani.