Local Bulletins

MAAFISA WA POLISI MJINI MARSABIT WAENDELEZA MSAKO WA POMBE HARAMU.

Na Caroline Waforo,

Maafisa wa polisi pamoja kwa ushirikiano na machifu wanaendeleza msako wa pombe haramu pamoja na mihadarati mjini Marsabit.

Operesheni hiyo iliyongo’a nanga alhamisi wiki jana inapania kuhakikisha kuwa utumizi wa pombe haramu pamoja na mihadarati unakomeshwa kikamilifu kulingana na kamanda wa polisi Leonard Kimaiyo.

Aidha wamiliki wa vilabu wametakiwa kutii sheria kwa kuhakikisha kuwa vilabu hivyo vinafunguliwa saa kumi na moja jioni na kufungwa saa tano usiku.

Anasema kuwa watakao kamatwa wakikiuka sheria  watawajibishwa kwa mjibu wa sheria.

Subscribe to eNewsletter