Local Bulletins

HOFU YASHUHUDIWA ENEO LA BALESA SARU, DUKANA – MARSABIT BAADA YA MAJAMBAZI WASIOJULIKA KUVAMIA ENEO HILO USIKU WA KUAMKIA LEO.

Na Grace Gumato

Hali ya wasiwasi inaendelea kushuhudia katika eneo la Qonye katika kata ndogo la Balesa Saru baada ya majambazi wasiojulika kuvamia eneo hilo usiku wa kuamkia leo na kujaribu kuiba ngamia.

Akizungumza na shajara ya Jangwani Katana Charo ambaye ni naibu kamishna wa Dukana amesema wajambazi hao walikuwa wamejihami na bunduki na waliweza kupiga risasi ndama ya ngamia katika tukio hilo.

Aidha Katana amehoji kuwa licha ya makabiliano hayo hakuna mtu yeyote amejeruhiwa au kuuawa hata hivyo amewarai wananchi kutokuwa na hofu kwani maafisa wa polisi wamesambazwa katika maeneo mbali mbali viungani mwa eneo hilo kushika doria.

Aidha amesema kuwa kiini kamili cha makabiliano hayo haikubainika mara moja kwani maafisa wa usalama wanaendelea na uchunguzi.

Hali hiyo inajiri wiki moja baada ya watu wanane kuuliwa kinyama na miili yao kuchomwa eneo la Elledimtu wadi ya Maikona na watu wanaoshukiwa kutoka taifa jirani la Ethiopia.

Subscribe to eNewsletter