Local Bulletins

DARA YA UVUVI MARSABIT YATAKIWA KUWEKA MIKATATI ITAKAYOSAIDIA UCHUKUZI KATIKA ZIWA TURKANA NA KUPUNGUZA AJALI ZA MASHUA KATIKA ZIWA HILO.

Na JohnBosco Nateleng’

Wito umetolewa kwa serekali ya kaunti ya Marsabit kupitia idara ya uvuvi imetakiwa kuweka mikatati ambayo itakuwa ikilinda uchukuzi unaoendelea katika ziwa Turkana ili kuweza kupunguza ajali za mashua zinazoshuhudiwa katika ziwa hilo.

Kwa mujibu wa aliyekuwa mwaniaji wa kiti cha MCA wadi wa Loiyangalani na ambaye pia ni mwanaharakati ya kutetea haki za binadamu katika eneo hilo Emmanuel Lotabo ni kuwa serekali bado haijaweka mikakati ambazo itasaidia wavuvi kuweza kufanya shughuli zao kwa njia salama na isiyo na hofu.

Lotabo ameitaka serikali kuhakikisha kuwa kuna mashua za dharura, katika ufuo wa ziwa Turkana, na pia kuhakikisha kuwa kila mashua ambayo inafanya uchukuzi ina koti la kuokoa Maisha (Life jacket) ambalo litasaidia iwapo ajali itatokea.

Kadhalika Lotabo amewachangamoto Wazazi pamoja na walezi kutowaruhusu Watoto kuenda ziwani haswa wakati wa likizo kwani inahatarisha Maisha yao kwa sababu huu ni mwaka wa tatu kwa jamii ya Loiyangalani kupoteza wanafunzi ambao wamemaliza masomo ya darasa la nane na kidato cha nne katika ziwa Turkana jambo ambalo  amesema linakera na kutia wasiwasi.

Lotabo ametoa rai kwa mashirika ya Mawasiliano, Safaricon na Airtel kuweza kuhakikisha kuwa wameboresha mawasiliano katika ziwa Turkana ili kuwafanya wavuvi kuripoti kisa chochote ambacho kitawatukia wakiwa katika shughuli zao za kila siku ziwani.

Wakti uo huo Wavuvi kutoka ziwa Turkana wametakiwa kuwa makini wanapoendeleza shughuli yao ya uvuvi katika ziwa hiyo kwani kumekuweko na mabadiliko ya anga ambapo upepo umekuwa mwingi katika eneo la Loiyangalani na maeneo mengine yanayokaribia ziwa Turkana.

Akizungumza na shajara ya radio Jangwani kwa njia ya simu, Steven Ekuwom ambaye ni mwenyekiti wa Lake Turkana BMUs Network amesema kuwa ni jukumu la kila mvuvi kuhakikisha kuwa amechukua tahadhari ya kulinda usalama wao majini haswa wakati huu ambapo mvua na upepo unashuhudiwa kwa wingi.

Hata hivo Ekuwom ameitaka serekali kuweza kubuni mbinu mbadala ya kuhakikisha kuwa wavuvi hawa wameelimishwa juu ya usalama wa bahari ili kuweza kuwakinga dhidi ya madhara yatokanayo na ukiukaji wa tahadhari zilizopo ziwani.

Subscribe to eNewsletter