Mwanaume moja wa miaka 38 ameponea kifo baada ya jaribio la kujitoa uhai kwa kujinyonga kutibuka usiku wa kuamkia leo katika kijiji cha Soweto mjini Laisamis kaunti ya Marsabit.
February 7, 2025
NA SAMUEL KOSGEI
Waandamanaji wanaoipinga serikali jijini Mombasa walichoma magari na kuharibu hoteli baada ya mtu mmoja mwenye bunduki kufyatulia risasi ovyo umati wa watu na kuwajeruhi takriban watu watatu.
Kulingana na walioshuhudia, mtu huyo anasemekana kukasirishwa na waandamanaji hao ambao walitatiza biashara katika Barabara ya Nyerere.
Kufuatia hali hiyo, magari kadhaa yaliharibiwa na majeruhi walikimbizwa hospitalini.
Wazima moto, hata hivyo, walifanikiwa kuzima moto huo.