Local Bulletins

Muthama akana madai kuwa vyama chini ya muungano wa Kenya Kwanza vimepanga namna ya kuwagawanya serikali.

Mwenyekiti wa chama cha UDA Johnstone Muthama.
Picha;Hisani

Na Samuel Kosgei,

Mwenyekiti wa chama cha UDA Johnstone Muthama amekana madai kuwa vyama chini ya muungano wa Kenya Kwanza wamepanga namna ya kuwagawanya serikali iwapo watashinda uchaguzi mkuu mwaka huu.

Muthama akizungumza na waandishi wa habari amesema kuwa vyama vya ANC, FORD KENYA na UDA hawajaelewana kwa chochote na badala yake yaliyoandikwa kwenye gazeti moja la humu nchini ni uvumi usiokuwa na msingi wowote.

Anasema kuwa chama cha UDA kitafanya uteuzi kote nchini kwa njia ya kidemokrasia pasi na kupendelea watu moja kwa moja.

Wakti uo huo aanasema kuwa yote yaliyosemwa kwenye gazeti hilo siku mbili zilizopita ni taarifa ambazo hazina ukweli kwani hawajaelewana kwa vyovyote vile.

 

Subscribe to eNewsletter