Local Bulletins

Wito Watolewa Kwa Wakaazi Wa Kaunti Ya Mandera Kupea Kipaumbele Maswala Ya Amani

Picha;Hisani

By Mark Dida,

Mshirikishi wa serikali kuu kanda ya kaskazini mashariki Nicodemus Ndalana ametoa wito kwa wakaazi wa kaunti ya Mandera kupea kipaumbele maswala ya amani baina ya jamii zinazoishi katika eneo hilo.

Haya yanajiri baada ya maafisa wa tume ya uwiano na utengamano ya NCIC pamoja na viogozi wa serikali ya kaunti na serikali kuu kuanzisha Mipango ya kuleta jamii za Garri na Murule pamoja katika kaunti hiyo kusuluhisha mgogoro ya mara kwa mara.

Aidha kamishna Ndalana ametaja kuwa iwapo umoja huo utadumu  atajivunia kwa miongoni mwa wakenya waliochangia amani hata katika ukanda huo hata baada ya kustafu.

Wakti uo huo Ametoa uwito kwa vijana wa kaunti ya Mandera kusomea kozi ya ualimu huku serikali ikiendelea na oparesheni dhidi kundi la kigaidi la Alshabab.

Subscribe to eNewsletter