Local Bulletins

Watahiniwa Kutoka Shule Za Kibinafsi Zilizofungwa Kwa Ajili Ya Makali Ya Korona, Hawatakosa Kukalia Mitihani Yao Ya KCSE Na KCPE – Magoha.

Waziri Wa Elimu Profesa George Magoha.
Picha;Hisani

By Waihenya Isaac.

Watahiniwa Kutoka Shule Za Kibinafsi Zilizofungwa Kwa Ajili Ya Makali Ya Korona, Hawatakosa Kukalia Mitihani Yao Ya KCSE Na KCPE Mwaka Ujao.

Kwa Mujubu Wa Wa Ziri Wa Elimu Profesa George Magoha Ni Kuwa Wizara Ya Elimu Pamoja Na Washikadau Katik Asekta Hiyo Wataandaa Kikao Ili Kutafuna Namna Ya Kuwasaidia Wanafunzi Hao.

Tayari Zaidi Ya Wanafunzi Elfu 56,000 Huenda Wakakosa Kuripoti Shuleni  Mnamo Siku Ya Jumatatu Tarehe 4 Baada Ya Shule 339 Za Kibinafsi Kufungwa Kufuatia Makali Ya Korona.

Aidha Waziri Magoha Ametaja kuwa Wizara Ya Elimu Itafanya Kazi Kwa karibu Na Wizara Zingine Husika Nchini Ili Kusuluhusha Changamoto Zitakazojiri.

Ripoti Za Hapo Awali Zilibaini Kuwa, Zaidi Ya Walimu 2,000 Na Wafanyakazi Wa Ziada 1,500 Watakosa Ajira Kufuatia Shule Walizokuwemo  Kufungwa.

Mwezi Septemba Mwaka Jana Serekali Ilifungua Shule Kwa Awamu Huku Wanafunzi Wa Gredi Ya Nne, Darasa La Nane Pamoja Na Kidato Cha Nne Wakiripoti Shuleni Kwa Muhula Wa Pili.

Subscribe to eNewsletter