Mtu mmoja afariki kutokana na ugonjwa wa Kalazaar Marsabit, sita wakipokea matibabu kulingana na serikali ya kaunti.
February 21, 2025
By Waihenya Isaac,
Shirika la kutetea haki za binadamu la Haki Afrika limetishia kuwashtaki maafisa wa polisi wanaowaachilia huru washukiwa wa dhulma za kijinisia.
Afisa wa shirika hilo Abdulrahman Mwangoka amewataka wakuu wa idara ya polisi kufuatilia suala hilo ili maafisa hao wakabiliwe kisheria.
Mwangoka ameshtumu vikali hulka ya maafisa wa polisi ya kuwaachilia huru washukiwa wanaotekeleza visa vya dhulma katika jamii.
Aidha ameahidi kushirikiana na shirika hilo ili kuzuia ongezeko la visa hivyo.
Amesisitiza hoja ya polisi kuwakamata na kuwachukulia hatua za kisheria washukiwa wa dhulma hizo.