Local Bulletins

Seneta Yusuf Haji Azikwa Hii Leo, Katika Maziara Ya Kiislamu Ya Lang’ata Jijini Nairobi

Picha;Hisani

By Samuel Kosgei

Wafanyakazi katika Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma Noordin Haji, ndio wa hivi punde kutuma risala za rambirambi kwa familia ya Seneta wa Garissa Yusuf Haji.

Wafanyakazi hao, kupitia ujumbe, wamempa pole-zao Noordin Haji kufuatia kifo cha babake asubuhi ya leo, na kumtaja kama balozi mkuu wa usalama na utangamano kote nchini.

Haji amezikwa saa kumi hii leo, katika Maziara ya Kiislamu ya Lang’ata jijini Nairobi, baada ya kumalizika sherehe ya maombi kwa ajili ya mwili wake, eneo la South C, Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine kuu serikalini wameudhuria hafla hiyo.

Usalama uliimarishwa katika barabara ya Lang’ata inayoelekea kwenye Maziaira hayo, msongamano wa magari mkubwa wa ukushuhudiwa eneo hilo.

Hawa hapa baadhi ya viongozi wakitoa rambirambi zao katika makazi yake Haji hii leo.

Subscribe to eNewsletter