Local Bulletins

Seneta Kipchumba Murkomen Kupinga Mipango Yoyote Ya Kumuondoa Seneta Irungu Kang’ata Kutoka Kwa Nafasi Yake Ya Kiranja Wa Bunge La Seneti

Picha; Hisani

By Adano Sharawe

Seneta Wa Elgeyo Marakwet Kipchumba Murkomen Sasa Anasema Atapinga Mipango Yoyote Ya Kumuondoa Seneta Irungu Kang’ata Kutoka Kwa Nafasi Yake Ya Kiranja Wa Bunge La Seneti

Murkomen Amesema Ikiwa Uongozi Wa Chama Cha Jubilee Utaitisha Kikao Cha Kumuondoa Kang’ata, Watahudhuria Na Kupinga Hatua Hiyo.

Amesema Badala Yake Wataondoa Wanachama Wasio Wa Chama Na Kukabidhi Nafasi Yao Kwa Wanachama Kamili.

http://

Kauli Yake Imejiri Baada Ya Madai Ya Kang’ata Kuwa Eneo La Mlima Kenya Haliungi Mkono Ripoti Ya BBI Kwenye Barua Yake Kwa Rais.

Seneta Wa Elgeiyo Marakwet Kipchumba Murkomen.
Picha; HisaniNi Madai Ambayo Yamepuuziliwa Mbali Na Viongozi Wa Eneo Hilo.

Magavana Walio Chini Ya Mwavuli Wa Kundi La Kiuchumi La Kaunti Za Eneo La Mlima Kenya, Wakiongozwa Na Mwenyekiti Wao Francis Kimemia Na Naibu Wake Gavana  Kiraitu Murungi Wa Kaunti Ya Meru, Walimkosoa Seneta Kangata Kwa Kukiuka Utaratibu Wa Kumzungumuzia Rais Uhuru Kenyatta Kupitia Vyombo Vya Habari.

Kwenye Taarifa Iliyotiwa Saini Na Magavana Kumi, Viongozi Hao Walimtaka Seneta Huyo Wa Murang’a Kuruhusu Wakenya Kushiriki Kwenye Mjadala Kuhusu Mchakato Wa BBI Ili Waweze Kufikia Uamuzi Wa Busara.

Subscribe to eNewsletter