Local Bulletins

Dereva aliyehusika katika ajali iliyowaua watu wawili hula hula Marsabit awasilishwa mahakamani.

Gari aina ya Probox lililoanguka katika eneo la Hula hula, Marsabit. Picha, Jangwani Fm

By Grace Gumato
Na katika mahakama hiyo hiyo ya Marsabit, dereva aliyehusika katika ajali ya Hulahula iliyowaua watu wawili amewasilishwa mahakamani.

Isaya Roble Elsimonte alifikiwa mbele ya hakimu Tom Mbayaki na kushtakiwa kwa mashataka ya mauaji ya kukusudia kwa kuendesha gari vibaya kinyume na sheria.

Elsimote alikamatwa siku ya Jumatatu wiki hii ikiwa ni wiki mbili tangu gari aina ya probox alilokuwa akiendesha kuhusika katika ajali na kusababisha vifo kule Hula Hula viungani mwa mji wa Marsabi kwenye barabara kuu ya Marsabit-Isiolo, tarehe 8 mwezi huu.

Gari aina ya Probox lililoanguka katika eneo la Hula hula, Marsabit. Picha, Jangwani Fm

Mshukiwa alifikishwa mbele ya hakimu Tom Mbayaki Wafula ambapo alikanusha mashtaka.
Hakimu Wafula alimuachilia kwa dhamana ya shilingi elfu ishirini kusubiri kusikizwa tena kwa kesi hiyo tarehe 12, Julai mwaka huu.

Subscribe to eNewsletter