Local Bulletins

Mamake Musalia Mudavadi, Hannah Atsianzale Mudavadi Aaga Dunia.

Mamake Musalia Mudavadi Hannah Atsianzale Mudavadi.
Picha; Musalia Mudavadi

By Waihenya Isaac & Jillo Dida

Mamake Aliyekuwa Kinara Wa ANC Musalia Mudavadi Hannah Atsianzale Mudavadi Ameaga Dunia.

Atsianzale Ameaga Dunia  Saa Kumi Na Moja Alfajiri Ya Leo Alipokuwa Akipokea Matibabu Katika Hospitali Ya Nairobi Akiwa Na Umri Wa Miaka 92.

Ripoti Kuhusiana Na Kifo Chake Zimewekwa Wazi Na Musalia Mudavidi Kupitia Mtadao Wa Twitter.

Katika Rambi Rambi Zake Wa Kutia Moyo, Rais Kenyatta Amemtaja Mama Hannah Kama Mchungaji Aliyejitolea, Mkarimu Na Mnyenyekevu Ambaye Alilea Familia Iliyofungamana Na Kuchangia Sana Maendeleo Ya Jamii Yake.

Huku Haya Yakijiri Mwakilishi Wa Kike Kaunti Ya Wajir Fatuma Gedi Anaomboleza Kifo Cha Babake Mzee Gedi Ali Kilichotokea Siku Ya Jumapili, Disemba 27.

Kifo Cha Mzee Gedi Kilitangazwa Mitandaoni Na Seneta Farhiya Haji Ambaye Pia Alikuwa Ametuma Rambi Rambi Zake Kwa Familia Ya Mwendazake.

Wakenya Na Viongozi Kadhaa Pia Waliomboleza Kifo Cha Mzee Gedi Kupitia Mitandao Ya Kijamii. 

Subscribe to eNewsletter