Mtu mmoja afariki kutokana na ugonjwa wa Kalazaar Marsabit, sita wakipokea matibabu kulingana na serikali ya kaunti.
February 21, 2025
Msimazi mkuu kwenye mbuga ya wanyama Marsabit national park Augustine Ajuoga amesema k.w.s katika kaunti ya Marsabit wanajiandaa vyema kwa siku ya kusherekea wanyama pori itakayofanyika mechi 3 mwezi ujao huku akihamasisha jamii kujua umuhimu wa kulinda wanyamapori pamoja na mazingira kwa manufaa yao.
Akizungumza na shajara ya radio Jangwani alipokuwa akifanya shughuli ya maandalizi ya siku ya kusherehekea wanyamapori duniani ama world wildlife day mwezi ujao ,Ajuaoga ameleezea umuhimu wa kutoa hamasisho kwa wanafunzi pamoja na jamii kwan ni jukumu na kila mmoja kulinda wanyamapori pamoja na mazingira.
Hafla hiyo imejumuisha wanafunzi kutoka shule ya gadamoji ambapo waliweza kuzuru mbuga hiyo ya wanyama mjini marsabit
Vile vile Augustine amesema ni jukumu la kila mwananchi kulinda wanyama pori pamoja na mazingira haswa akiwahimiza wakaazi wa marsabit kuwa mstari wa mbele katika kulinda mazingira kwani ina manufaa kwa jamii kwa jumla
Aidha, amesema kuwa ni sharti wakaazi wa marsabit watembelee mbuga ya wanyama huku akiwahakishia usalama wao .