Mtu mmoja afariki kutokana na ugonjwa wa Kalazaar Marsabit, sita wakipokea matibabu kulingana na serikali ya kaunti.
February 21, 2025
Wakaazi katika kaunti ya Marsabit wamesherehekea siku ya wapendanao kwa njia mbalimbali.
Wakiongea na kituo hiki mjini Marsabit baadhi ya wakaazi wamesema kuwa siku hii ni spesheli sana tuu kwa wapenzi lakini pia kwa watu muhimu katika jamii. Hata hivyo wengi wao wanasema kuwa hali ya uchumi imesababisha wengi kutoisherehekea siku hii spesheli ya valentines.
Ni siku inayosherehekewa katika maeneo mengi duniani ambapo watu huzawadiana maua, kadi za mapenzi na zawadi nyingine muhimu kwa wanaowaenzi.
Wakati huo wanabiashara wanaojihusisha na bihdaa za zawadi za kimapenzi wanasema kuwa leo ndio siku yao muhimu kwani wateja wameongezeka kwa kiwango kikubwa.