Local Bulletins

Hatua ya benki za kibiashara nchini kupunguza riba ya mkopo yapongezwa na wataalamu wa kifedha.

Na Moses Sabalua.

Hatua ya benki kuu nchini CBK kutaka benki za kibiashara nchini kupunguza riba ya kupeana mkopo imepongezwa na kutajwa kama njia mojawapo ya kuinua wanabiashara na biashara zao.

Mtaalam wa kifedha katika kaunti ya Marsabit John Maina amesema hatua ya Benki kuu ya Kenya kushusha riba kutoka asilimia 16.5 hadi asilimia 14 itasaidia pakubwa katika kuinua biashara na uchumi humu nchini .

Akizungumza na shajara ya Radio Jangwani amesema punguzo hilo la riba litasaidia pakubwa katika  kupanua  biashara na itasaidia  wananchi kuchukua mikopo  kwa bei rahisi na itainua uchumi humu nchini pamoja na kubuni ajira kwa wananchi.

Subscribe to eNewsletter