County Updates, Local Bulletins

Ni watu 129 pekee ambao wamesajiliwa kama wapiga kura katika kaunti ya Marsabit katika zoezi jipya linaloendelea kwa sasa la kuwasajili wapiga kura.

Meneja wa IEBC tawi la Marsabit Festus Murithi.
Picha;Radio Jangwani

By Mark Dida,

Ni watu 129 pekee ambao wamesajiliwa kama wapiga kura katika kaunti ya Marsabit katika zoezi jipya linaloendelea kwa sasa la kuwasajili wapiga kura.

Kwa mujibu wa meneja wa tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC tawi la Marsabit Festus Murithi, nikuwa 129 hao wamesajiliwa tangu zoezi hilo kungoa nanga tarehe 14 mwezi huu huku zoezi la kuhamasisha umma kuhusiana na maswala ya uchaguzi pamoja na kuhimiza raia kujisajili kamawapiga kura likiendelea.

Murithi amebaini kuwa shughuli hiyo inaendelea katika kaunti zote nne ndogo za Marsabit.

Kulingana na Murithi ni kuwa mfumo huo unalenga kuhamasisha umaa na kuupa elimu ya kutosha, kuhusu haki ya kusajiliwa na umuhimu wa kushiriki kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2022.

Ameogeza kuwa shughuli hiyo ya kuhamasisha umma huandaliwa  kila mwaka ila mwaka 2020 ilitatizwa na janga la corona lililotatiza shughuli nyingi.

Wakti uo huo Murithi ametaja changamoto ya usalama na umbali wa kimaeneo katika kaunti ya Marsabit kama kizungumkuti katika kutelekeza kazi yao.

Amehoji kuwa kunao wakaazi waliohama kwao kufuatia hofu ya usalama hivyo kuwafikia mashinani ikiwa changamoto nyigine.

 

 

Subscribe to eNewsletter