Highlights

Walimu 459 kutoka shule za JSS wapata mafunzo ya kidijitali kaunti ya Marsabit

Na Sabalua Moses

Zaidi   ya walimu 459 kutoka shule za sekondari msingi JSS wanaendelea kupokea  mafunzo ya kidijitali  katika kaunti ya Marsabit

Haya ni kwa mujibu wa mkurugenzi mkuu wa tume ya kuajiri walimu kaunti ya Marsabit Hussein Abdi akizungumza  na wanahabari katika shule ya S.K.M  

Hussein amesema mpango huo unapanga kuboresha masomo ya mtaala  wa CBE pamoja na kusaidia walimu   katika mifumo ya kidijitali katika kupata maudhui ya masomo yao na usalama wa mitandao katika mtaala wa CBE.

Mafunzo hayo yanajiri serikali kuu ikiendelea kuhakikisha kuwa  mtaala   wa  CBE unaboreshwa  nchini.

 Vile vile kwa upande wake mwalimu Dennis Munene kutoka shule ya Chalbi Muslim amesema mafunzo hayo ya kidijitali itawasaidia walimu katika kupanga masomo yao na kuboresha masomo ya mtaala wa CBE.

Aidha ,kwa upande  wake Clarkson Cheruyiot naibu afisa wa kidijitali ICTA  mamlaka ya teknolojia ya habari na mawasiliano amesema  kufikia mwisho wa mafunzo haya walimu watakuwa na  uwezo wa kutumia masomo hayo  ya dijitali kuboresha masomo yao shuleni.

Mafunzo hayo yamewaleta walimu kutoka kaunti ndogo ya Marsabit Central,Laisamis,Chalbi na Loyangalani

Radio Jangwani 106.3FM is a community radio station situated in Marsabit County broadcasting from Marsabit town. It is the brain child of the bishop of catholic diocese of Marsabit, Rt. Rev. Peter Kihara. It is established with the objective of reaching the people Marsabit diocese and Marsabit County for evangelization, Education, entertaining and disseminating information to the masses.

Post Comment