Marsabit yasalia tulivu wakati wa maandamano ya kumbukumbu ya Gen-Z
Na Abdiaziz Yusuf
Huku maandamano ya kumbukumbu ya vijana wa Gen-Z yakishuhudiwa katika maeneo mbalimbali nchini, kaunti ya Marsabit imesalia tulivu bila usumbufu wowote.
Baadhi ya vijana waliozungumza na shajara wamesema kuwa maandamano yanapoteza muda na kuathiri shughuli za kujitafutia riziki, hasa wakati ambapo gharama ya maisha imeendelea kuwa juu.
Aidha wamesema badala ya kushiriki maandamano watawasilisha ujumbe wao kupitia sanduku la kura wakati wa uchaguzi.
Hata hivyo vijana hao wamehimizana kujitokeza kwa wingi wakati wa uchaguzi ili kuchagua viongozi wenye maono ya kuiletea nchi maendeleo bila kujali kabila au matabaka ya kijamii.



Post Comment