Wakazi wa Golole wanufaika na ujenzi wa mnara wa mawasiliano
Na Nyabande Orwa
Wakazi wa eneo la Golole wadi ya Uran wanakilasababu ya kutabasamu baada ya mnara wa mawasiliano. Wakizungumza na kituo hiki wakazi hao wamesema hatua ya kuwekewa mnara huo utawasaidia katika mawasialiano na kuboresha eneo hilo kimaendeleo.
Vile vile wakazi hao wakizungumza na kituo hiki wanasema tangia Kenya kujipatia uhuru hawajakuwa na huduma za mawasiliano suala lililowatenga na maeneo mengine ya kaunti hii ya Marsabit.
Wakati uo huo wameipongeza serikali kwa juhudi za kuweka mnara huo. Vile vile wamesema sasa huduma za matibabu na elimu zitaboreka kwa wanafunzi wanaotegemea kusoma kupitia mtandao. Ni uzinduzi uliofanywa na katibu katika wizara ya kawi na nishati Kello Harsama.



Post Comment