Highlights

Sampuli za maji zachukuliwa kufuatia vifo vya ng’ombe Korr

Na Abdiaziz Yusuf

Wasiwasi umetanda katika eneo la Korr, kaunti ndogo ya Ngurnet, kaunti ya Marsabit, baada ya ng’ombe saba kufariki dunia wakidaiwa kunywa maji kutoka kwenye kisima kilichopo eneo hilo.

Hata hivyo, chanzo halisi cha vifo hivyo bado hakijafahamika, huku uchunguzi ukiendelea.

Akizungumza na Shajara ya Radio Jangwani, mwakilishi wa wadi ya Korr, Daudi Tomasot, amesema sampuli za maji kutoka kisima hicho tayari zimechukuliwa na kupelekwa katika maabara ya serikali kwa uchunguzi ili kubaini iwapo maji hayo ndiyo yaliyosababisha vifo vya mifugo hiyo.

Tomasot amewataka wafugaji kuwa waangalifu na kusubiri matokeo ya uchunguzi kabla ya kuendelea kutumia maji kutoka kwenye kisima hicho. Ameongeza kuwa serikali itatoa taarifa rasmi mara tu matokeo ya uchunguzi yatakapokamilika.

Post Comment