Rais Ruto ahakikishia taifa uchaguzi wa haki na salama mwaka ujao.
Na Samuel Kosgei
Rais William Ruto amejitosa katika mjadala unaoendelea kuhusu iwapo atahudumu kwa muhula mmoja au miwili, akieleza imani kuwa Kenya itafanya uchaguzi wa amani, huru na wa haki huku akiwataka Wakenya kuendelea kuzingatia umoja na maendeleo ya taifa.
Akizungumza wakati wa hafla ya maombi jijini Nairobi hii leo, Rais alisema serikali yake imejitolea kuendeleza ajenda ya mageuzi ya kitaifa kuelekea uchaguzi mkuu ujao, akisisitiza kuwa taratibu za kidemokrasia zitaheshimiwa na kulindwa.
Rais alisema masuala ya matokeo ya kisiasa, ikiwemo hatma yake ya kisiasa, yako mikononi mwa Mungu, huku akiwataka Wakenya kudumisha utulivu na kuepuka siasa za mgawanyiko.
Aidha, alikashifu juhudi zozote za kueneza migawanyiko kabla ya uchaguzi, akionya kuwa majaribio ya kuvuruga umoja wa taifa hayatofaniki



Post Comment