Highlights

Nyingi ya shule Marsabit kutoa mafunzo ya STEM na Sayansi ya Kijamii huku Sanaa na Spoti ikitajwa kuwa na changamoto ya muundo msingi.

NA SAMUEL KOSGEI

Shule nyingi kwenye gredi ya 10 hadi 12 katika kaunti ya Marsabit zitatoa masomo ya CBE katika njia mbili ambayo ni (STEM) na Sayansi ya Kijamii yaani Social Sciences.

Katibu wa chama cha walimu wa shule za sekondari KUPPET Sarr Galgalo, ameambia shajara kuwa shule nyingi hapa Marsabit hazina muundo msingi nzuri ya kutoa mafunzo ya Sanaa na Sayansi ya michezo kama inavyotakiwa na idara ya elimu nchini.

Anasema kutokana na changamoto hiyo itakuwa vigumu kwa shule nyingi humu jimboni kusomesha somo la Sanaa na sayansi ya Michezo.

STEM inajumuisha masomo kama vile Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati.

Hata hivyo anasema kuwa wizara ya elimu imewakikishia kuwa matayarisho yote yako vizuri kwa ajili ya kupokea wanafunzi wa gredi ya 10 January mwakani.

Radio Jangwani 106.3FM is a community radio station situated in Marsabit County broadcasting from Marsabit town. It is the brain child of the bishop of catholic diocese of Marsabit, Rt. Rev. Peter Kihara. It is established with the objective of reaching the people Marsabit diocese and Marsabit County for evangelization, Education, entertaining and disseminating information to the masses.

Post Comment