County Updates

Serekali ya Kaunti ya Marsabit Kuwaajiri Walimu wa ECDE Kwa Mkataba wa Kudumu

Waziri wa Elimu kaunti ya Marsabit Bi. Ambaro Ali

Na Isaac Waihenya

Serekali ya kaunti ya Marsabit inaandaa mikakati ya kuwaajiri walimu wa chekechea (ECDE) kwa mkataba wa kudumu.

Hayo ni kwa mujibu wa Waziri wa Elimu katika kaunti ya Marsabit Bi. Ambaro Abdulla Ali.

Akizungumza wakati wa kufunzu kwa zaidi ya walimu 230 wa shule za chekechea katika tasisi ya Tendo Valley College hapa mjini Marsabit, waziri Ambaro alitaja kwamba serekali ya kaunti imejiza titi kuhakikisha kuwa shule za chekechea jimboni zina walimu wa kutosha.

Aidha waziri Ambaro alifichua kuwa, wiki hii seerkali itaanza zoezi la kuwapiga msasa walimu wa nyanjani ya Interns ili kutatuta kero la ukosefu wa walimu katika baadhi ya shule hapa jimboni Marsabit.

Subscribe to eNewsletter