Mwanaume moja wa miaka 38 ameponea kifo baada ya jaribio la kujitoa uhai kwa kujinyonga kutibuka usiku wa kuamkia leo katika kijiji cha Soweto mjini Laisamis kaunti ya Marsabit.
February 7, 2025
By Samuel Kosgei,
Wazazi Wa Wanafunzi Wanaoishi Katika Kaunti Ndogo Ya Loiyangalani Wameombwa Kufanya Hima Kuwarejesha Wanao Shuleni Kabla Hatua Kali Za Kisheria Kuchukuliwa Dhidi Yao.
Naibu Kamishna Wa Eneo Hilo Stephen Mavina Akizungumza Na Kituo Hiki Amesema Kuwa Bado Kuna Changamoto Wanayokumbana Nayo Kuhakikisha Kuwa Watoto Wote Wanarudi Shuleni Haswa Ikichangiwa Na Uwepo Wa Mila Na Wengine Kujihusisha Na Uchungaji Wa Mifugo.
Ametoa Onyo Kwa Wale Ambao Hawatakua Wamewapeleka Wanao Shuleni Kufukia Jumatatu Kuwa Watashtakiwa Ikizingatiwa Kuwa Ni Haki Ya Kila Mtoto Kupata Elimu.
Kwenye Suala La Maji Kusambaa Hadi Ktika Shule Ya Msingi Ya Elmolo Viungani Mwa Ziwa Turkana, Mavina Amesema Kuwa Kufikia Sasa Hali Ni Afueni Ikilinganishwa Na Wiki Mbili Zilizopita Shule Zilipokuwa Zinafunguliwa.