County Updates, Diocese of Marsabit, Local Bulletins

Kamishna Paul Rotich Awahakikishia Wakaazi Wa Kaunti Ya Marsabit Usalama Wa Kutosha.

Kamishna Wa Kaunti Ya Marsabit Paul Rotich.
Picha;Hisani

By Waihenya Isaac

Kamishna wa kaunti ya Marsabit Paul Rotich amewahakikishia wakaazi wa kaunti ya Marsabit usalama wa kutosha.

Akizungumza wakti wa Uzinduzi wa shihena ya Chakula cha msaada Kutoka kwa shirika la msaba mwekunduku uliofanyaika hapa mjini Marsabit,Kamishna Rotich ametaja kuwa serekali inafanya kila jitihada ili kuondoa kero la ukosefu wa usalama jimboni.

Vilevile Rotich ameshukururu mashirika ya kijamii pamoja na lile la Msalaba mwekundu kwa kuwa katika mstari kwa kwanza kuwajali wananchi wa kaunti hii haswa kipindi cha jalali.

Kwa upande wake katibu mkuu wa shirika la Msalaba mwekundu hapa nchini Bi. Asha Mohammed ni kuwa  zaidi ya watu 147,000 wanahitaji msaada wa  chakula hapa jimboni huku shirika hilo likilenga watu 47,000 katika awamu  ya kwanza.

Asha amesema kuwa Shirika hilo pia linafanya kazi kwa pamoja na serekali ya kaunti ili kutatua tatizo la ukosefu wa maji.

Aidha Asha amesema kuwa siku za usoni, Shirika hilo litalenga kuwapa wananchi fedha kuliko vyakula ili waweze kushughulika mahitaji yao wenyewe.

Subscribe to eNewsletter