County Updates

MILIONI 91 KWA KAUNTI YA MARSABIT KUKABILI JANGA LA VIRUSI VYA CORONA.

Maafisa wakuu wa usalama kaunti ya Marsabit wakiong0oza zoezi la ukaguzi na upimaji wa virusi vya corona katika kaunti ndogo ya Moyale.

By Jillo Dida

Kaunti ya marsabit imefadhiliwa shilingi millioni 91 na serikali kuu kusaidia wasio jiweza katika jamii wakti uchumi ya kenya ikiendea kusambaratishwa na mambukizi ya virusi vya corona. Aidha kwa mujibu wa kamishna wa jimbo hili Evans Achoki fedha hizo zitatumika kusaidia wazee wa miaka sabini na zaid pamoja na walemavu. Tayari shilingi millioni 32 imewekwa kando kulipa watoto yatima 468 katika kaunti hii ya marsabit, Vile vile amesema kuwa wazee wa miaka sabini na zaidi 6870 pia wameorodheshwa kupokea fedha hizo pamoja na walemavu 557 kote jimboni. Mengi zaidi

Subscribe to eNewsletter