Local Bulletins

Watu watatu waaga dunia wengine wanane wakijeruhiwa Malgis, Marsabit

Lori lililoanguka na kusababisha mauaji

Na Machuki Dennson

Watu watatu waliaga dunia Alhamisi jioni baada ya kuhusika katika ajali ya barabarani eneo la Malgis hapa Marsabit.

Watu wanane wamejeruhiwa katika ajali hiyo akiwemo dereva wa lori la kubeba mchanga.

Kulingana na dereva wa Lori hilo, ni kwamba gurudumu Moja la lori hilo lilitoka ghafla na hivyo kusababisha lori hilo kuanguka.

Watatu walioaga dunia walikuwa ndani ya lori Hilo upande wa nyuma japo Lori hilo halikuwa na mchanga.

Polisi kutoka kituo Cha Laisamis ambao walifika eneo hilo muda mfupi kabla ya saa kumi na mbili jioni wamewapeleka majeruhi hospitalini Laisamis.

 

Subscribe to eNewsletter