Local Bulletins

Rais Kenyatta Kuhutubia Taifa Hii Leo Kuhusu Hali Ya Maambukizi Ya Korona

 

Rais  Uhuru Kenyatta, Picha;Hisani

By Waihenya Isaac,

Rais Uhuru Kenyatta anatarajiwa kuhutubia taifa hii leo kuhusu hali ya maambukizi ya korona na mikakati mipya ambayo serikali inaweka kudhibiti maambukizi zaidi.

Hata Hivyo upo uwezekano kwamba Rais huenda akakaza kamba kwenye masharti ya kuzuia msambao wa virusi hivyo.

Hotuba ya rais inajiri wakati taifa linakabiliana na wimbi la tatu la maambukizi ya korona.

Aidha Rais anatarajiwa kupiga marufuku mikutano ya kisiasa, kuongeza muda wa kafyuu inayoanza saa nne usiku huku ikiarifiwa kwamba huenda akafunga tena maeneo ya burudani kufuatia kuongezeka kwa msambao wa virusi hivyo.

Hiyo jana watu 829 walipatikana na virusi hivyo kati ya sampuli 6,239 zilizopimwa na kufikisha idadi ya jumla ya maambukizi nchini kuwa 111,185.

Subscribe to eNewsletter