Local Bulletins

Kizaazaa Chazuka Kaunti Ya Meru Wakati Ambapo Waakilishi Walikuwa Wakihamasisha Wenyeji Kuhusiana Na Mswada Wa BBI.

Picha;Hisani

By Adano Sharawe,

Kizaazaa kilizuka kaunti ya Meru wakati ambapo waakilishi walikuwa wakihamasisha wenyeji kuhusiana na mswada wa BBI.

Mkutano wa umma ulioandaliwa katika ukumbi wa Kamunde mjini Meru ulitibuka baada ya waakilishi wadi kushindwa kuwashawishi wenyeji kuunga mkono marekebisho ya katiba.

Kiongozi wa wengi kaunti ya Meru Victor Kareithi alijaribu kuwatuliza waliohudhuria ila hakuweza na waakilishi wadi hao wakalazimika kusitisha mkutano.

Wakazi wa Meru wanaendelea kutoa hisia tofati huku wengine wakiomba serikali kuogeza muda zaidi ili kupata nafasi ya wao kuisoma na kuielewa ripoti hiyo.

Subscribe to eNewsletter