Local Bulletins

Wizara Ya Fedha Yasema Ipo Tayari Kutoa fedha Za Kufanikisha Mchakato Wa Kura Ya Maoni (BBI).

Waziri Wa Fedha Ukur Yattani.
Picha;Hisani

By Samuel Kosgei.

Wizara ya fedha imesema kuwa iko tayari kutoa fedha za kufanikisha mchakato wa kura ya maoni kupitia mapendekezo ya BBI.

Waziri wa hazina ya kitaifa Ukur Yatani amesema kuwa serikali haiwezikosa fedha za kufanikisha zoezi katika suala la linalochukulia kwa uzito na kipaumbele.

Tume ya uchaguzi na mipaka IEBC awali ilisema kuwa kufanikishwa kwa kura ya maonitume hiyo itahitaji shilingi bilioni 14 ila kinara wa chama cha ODM Raila Odinga alikosoa hitaji hilo la IEBC akisema kuwa IEBC inahitaji shilingi bilioni 2 pekee.

Wiki jana wizara ya fedha iliidhinisha shilingi bilioni Sh93.7 za kutumika kudhibitisha sahihi milioni 4.4 zilizokusanya ili kuwezesha mchakato wa mswada wa BBI 2020.

Yattani ameongeza kuwa BBI kwa sasa ni suala la kipaumbele ikizingatiwa kuwa itasaidia uchumi wa nchini kuimarika.

Subscribe to eNewsletter