Wazazi wote Loglogo wametakiwa kupeleka wanao shuleni kufuatia amri ya rais.
Na Samuel Kosgei
Wazazi wote katika lokesheni ya Loglogo iliyo katika kaunti ndogo ya Laisamis wametakiwa kuhakikisha kuwa watoto wote waliomaliza gredi ya 9 wanajiunga na gredi ya 10 kama ilivyoamrishwa na serikali.
Wito huo umetolewa na chifu wa lokesheni ya Loglogo Andrew Korole aliyewataka watoto wote wapelekwe shule bila kuzingatia uwezo wao wa kifedha kwani kila mmoja ana haki ya kupokea elimu kulingana na katika ya nchi.
Hata hivyo amekiri kuwa baadhi ya wafugaji wanapitia changamoto katika kupata bei nzuri ya mifugo wanapouza ili kutafuta karo za shule.



Post Comment