Highlights

Ukeketaji imetajwa kuwa mojawapo ya sababu ya ugonjwa wa fistula Marsabit.

Na Samuel Kosgei

2223

Akizungumza katika hafla ya kujadili mbinu za kukabiliana na dhuluma za kijinsia na kuhamasisha haki za mtoto msichana, Bokayo amesema kuwa ukeketaji (FGM) kwa kiasi kikubwa huchangia tatizo la wanawake kushindwa kuzuia mkojo au haja kubwa, hali inayojulikana kama fistula.

Suala lingine kuu linalochangia shida hiyo ni wasichana kuolewa wangali wadogo na wanapojifungua hupitia hali ngumu kwani viungo vya mwili bado havijakomaa.

Amewahimiza wanawake waliohudhuria kikao hicho kusaidia kueneza ujumbe wa kupinga na kutokomeza ukeketaji wa wasichana, akisisitiza kuwa mila hiyo ni kinyume na haki za binadamu na inaleta madhara makubwa kiafya.

Wito wake unajiri siku moja baada ya ulimwengu kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake jana, Jumapili.

Radio Jangwani 106.3FM is a community radio station situated in Marsabit County broadcasting from Marsabit town. It is the brain child of the bishop of catholic diocese of Marsabit, Rt. Rev. Peter Kihara. It is established with the objective of reaching the people Marsabit diocese and Marsabit County for evangelization, Education, entertaining and disseminating information to the masses.

Post Comment