Highlights

Serikali ya kaunti ya marsabit kuimarisha mpango wa chakula shuleni kwa watoto wa chekechea

NA JB Nateleng

Huku hali ya ukame ikizidi kushuhudiwa katika kaunti ya Marsabit, serekali ya kaunti kupitia idara ya elimu imesema kwamba inawekeza juhudi za kuhakikisha kwamba Watoto wa shule za chekechea wanabakia shuleni kupitia mpango wa kuwapa chakula shuleni.

Idara hii kupitia waziri Ambaro Abdulahi imesema kwamba usambazaji wa chakula umecheleweshwa muhula huu na mchakato wa ununuzi ambayo serekali ilikuwa ikifuatilia huku wakitaka wazazi kuwapeleka wanao shuleni.

Wamesema kwamba mchakato wa ununuzi umemalizika na huenda wakasambaza chakula kwa shule tofauti mapema wiki ijayo.

Post Comment