Mtoto wa chini ya siku 3 apatikana ametupwa kando ya barabara, Marsabit Central
NA Sabalua Moses
Mtoto wa chini ya siku tatu amepatikana akiwa ametupwa kando ya barabara katika eneo la Riverside kaunti ndogo ya Marsabit Central.
Akithibitisha kisa hicho cha Jumanne jioni, OCPD wa Marsabit Central Beethoven Gachago, amesema kuwa msamaria mwema alimpata mtoto huyo wa kike akiwa amefungwa na mavazi na kupiga ripoti katika kituo cha polisi.
Ripoti hiyo pia iliwasilishwa katika idara ya watoto.
Mtoto huyo yuko katika hali nzuri na anaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya Rufaa na Mafunzo ya Marsabit, kabla ya kupelekwa katika makao salama.
OCPD Gachago ametoa wito kwa umma kutoa ripoti yoyote kuhusu mama ya mtoto huyo huku pia mzazi huyo akiombwa kujiwasilisha kituoni.



Post Comment