Miti milioni 30 kupandwa Badhauri kukuza uhifadhi wa mazingira
Msimamizi mkuu wa misitu katika kaunti ya Marsabit, Kenneth Muthuri, amesema idara yake kwa ushirikiano na serikali ya kaunti inalenga kupanda takriban miti milioni 30 katika eneo la Badhauri kama njia ya kurejesha misitu ya asili na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Akizungumza na kituo hiki wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, Muthuri amesema Marsabit bado iko nyuma katika kiwango cha uoto wa misitu, huku maeneo yenye misitu yakichukua asilimia 2.6 pekee ya eneo lote la kaunti. Ameeleza kuwa uchomaji wa makaa ndio chanzo kikuu cha uharibifu wa miti katika eneo hilo.
Muthuri amewataka wakazi kushirikiana na serikali katika juhudi za kuhifadhi mazingira kwa kushiriki kikamilifu katika upanzi wa miti, si tu kwenye maeneo ya umma bali pia katika makazi yao.



Post Comment