Maafisa wa kliniki marsabit waanza mgomo baada ya mazungumzo kugonga mwamba
NA Sabalua Moses
Maafisa wa kliniki kaunti ya Marsabit wamerudi mgomoni siku ya tatu mfululizo sasa baada ya mazungumzo yao na serikali ya kaunti kugonga mwamba.
Mgomo huu unakuja takriban siku 30 baada yamaafisa hao wa kiliniki kurejea kazini kutokana na amri ya mahakama ya Nyeri iliyositisha mgomo wao uliopita, wameamua kuendelea na mgomo baada ya pande husika kushindwa kufikia makubaliano.
Kwa mujibu wa barua ya muungano wa maafisa wa kliniki, mgomo umechochewa na mishahara duni, mazingira magumu ya kazi, na kutopandishwa cheo.



Post Comment