Jamaa afikishwa mahakamani Marsabit kwa tuhuma za kutishia kumwangamiza mwenzake.
NA NYABANDE ORWA
Jamaa mmoja amefikishwa katika Mahakama ya Marsabit kwa tuhuma za kumtishia mwenzake kumwangamiza yeye na watoto wake.
Mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya Marsabit, Simon Arome, mshukiwa Hussein Sode anatuhumiwa kutoa matamshi ya vitisho dhidi ya mlalamishi Dade Adan katika lokesheni ya Nagayo tarehe saba mwezi huu wa Desemba, akidaiwa kusema kuwa angemdunga kisu yeye pamoja na familia yake.
Katika shtaka la pili, mshukiwa Sode anatuhumiwa kutumia maneno ya matusi dhidi ya mlalamishi kama njia ya kumdhalilisha.
Hata hivyo, mshukiwa amekana tuhuma zote dhidi yake.
Kesi hiyo inatarajiwa kutajwa tena tarehe 13 mwezi ujao wa Januari mwakani.



Post Comment