Local Bulletins

Naibu Wa Rais Dkt William Ruto Awakashifu Wanasiasa Kwa Kuweka Maslahi Yao Mbele Wakti Huu Wahudumu Wa Afya Wanapogoma.

Naibu Wa Rais William Ruto Akihutubu Jijini Nairobi.
Picha; Hisani

By Samuel Kosgei,

Naibu Wa Rais Dkt William Ruto Amejitokeza Na Kukashifu Vikali Wanasiasa Anaosema Kuwa Wanaweka Maslahi Yao Mbele Haswa Wakti Huu Wahudumu Wa Afya Wanapogoma.

Akizungumza Katika Kaunti Ya Kericho Alipohudhuria Mazishi Ya Luteni Mstaafu John Koech, Ruto Anasema Kuwa Taifa Lipo Kwenye Janga Kuu La Kimataifa Na Hivyo Kusema Kuna Haja Ya Nchi Na Viongozi Wote Kushughulikia Kero La Virusi Vya Corona Badala Ya Siasa Za Mvutano.

Anasema Ili Taifa Lifaulu Katika Mapambano Ya Corona Ni Sharti Msalahi Ya Madaktari Na Wauguzi Yashughulikiwe Mwanzo.

Ruto Ameonekana Kumlenga Kinara Wa Chama Cha ODM Raila Odinga Aliyedai Hapo Jana Kuwa Madaktari Wanafaa Kusubiri Uchumi Uimarike Kabla Ya Wahudumu Kuitisha Nyongeza Ya Marupurupu.

Kwenye Hafla Hiyo Ruto Aliandamana Waziri Wa Kawi Charles Keter, Gavana Wa Kericho Prof Paul Chepkwony, Naibu Gavana Wa Kericho Susan Kikwai, Seneta Aaron Cheruiyot (Kericho) Sawia Na Seneta Kipchumba Murkomen (Elgeyo Marakwet).

Wengine Walioandamana Naye Ni Seneta Millicent Omanga, Silvanus Maritim (Ainamoi), Johana Ng’eno (Emurua Dikirr), Nelson Koech (Belgut) Na Geoffrey King’ang’i (Mbere South).

Wito Wa Kujilinda Dhidi Ya Virisi Vya Corona Imetiliwa Mkazo Na Waziri Keter Aliyeoma Wakenya Kuzingatia Sharia Za Wizara Ya Afya.

 

Subscribe to eNewsletter