Bwawa la Bakuli kutosheleza maji kwa kipindi cha miwezi miwili tu-MARWASCO yasema
NA Caroline Waforo
Huenda hali ya uhaba wa maji ikawa mbaya zaidi katika kaunti ya Marsabit, kutokana na athari za kiangazi kinachoshuhudia jimboni kufuatia kufeli kwa mvua za msimu wa mwezi October, November na December mwaka jana.
Kulingana na John Halkano Guyo ambaye ni afisa katika kampuni ya kutoa huduma za maji na majitaka kaunti ya Marsabit MARWASCO, bwawa la Bakuli linaweza kutosheleza mahitaji ya maji kwa kipindi cha miezi miwili tu ijayo.
Amesema kuwa kwa sasa kampuni hiyo inalazimika kuwapa wananchi maji kwa vipimo ili kuhakikisha kuna usawa na utoshelevu wa maji yaliyopo.



Post Comment