Wauzaji wa samaki katika eneo la Loyangalani wataka msaada wa soko wa kuuzia samaki wao.
Na Sabalua Moses
Mwenyekiti wa kikundi cha akina mama cha Kilimabogo Fried Fish Fransesca Lopeyok amesema kuwa ukosefu wa soko la kuuzia samaki ndio changamoto kuu kwa wachuuzi wa samaki katika kikundi hicho cha akina mama eneo la Loiyangalani.
Akizungumza na shajara ya Radio jangwani kwa njia ya simu Fransesca amesema kuwepo kwa soko kwa kikundi hicho kutawasaidia kuuza samaki pamoja na kupata wanunuzi kwa urahisi.
Aidha ,Fransesca amesema ukosefu wa soko wa samaki imekuwa changamoto kwao akitaka serikali na wahisani kuwasaidia kujenga soko hilo.



Post Comment