Highlights

Wananchi Marsabit watakiwa kuchukua tahadhari wakati huu idara ya MET imetabiri mvua katika baadhi ya maeneo

Na Caroline Waforo

Wakaazi katika kaunti ya Marsabit wametakiwa kuchukua tahadhari wakati huu ambapo idara ya hali ya anga nchini MET imetabiri kuwa maeneo mengi jimboni yataendelea kupokea mvua.

Ni tahadhari ambayo imetolewa na kamanda wa polisi kaunti ya Marsabit Leonard Kimaiyo ambaye pia amewataka wananchi kuepuka mikondo ya maji ili kuepuka hatari.

Vilevile madereva wametakiwa kuwa waangalifu barabarani kutokana na ukungu unaoshuhudiwa hasa nyakati za asubuhi huku Kamanda Kimaiyo akiwataka wananchi kuripoti visa vyovyote wakati huu wa mvua.

MET imetabiri kuwa baadhi ya maneo jimboni yatapokea mvua asubuhi, mchana na mvua inayoambatana na ngurumo nyakati za usiku.

Radio Jangwani 106.3FM is a community radio station situated in Marsabit County broadcasting from Marsabit town. It is the brain child of the bishop of catholic diocese of Marsabit, Rt. Rev. Peter Kihara. It is established with the objective of reaching the people Marsabit diocese and Marsabit County for evangelization, Education, entertaining and disseminating information to the masses.

Post Comment