Highlights

Wachimba migodi waonywa dhidi ya uchimbaji haramu wa dhahabu katika machimbo ya Dabel

NA Caroline Waforo

Wachimba migodi wanaoendelea na shughuli za kusaka dhahabu kwa njia haramu katika migodi ya Hillo eneobunge la Moyale Kaunti ya Marsabit, wametakiwa kuondoka mara moja hadi wakati ambapo serikali itatoa mwongozo wa kufunguliwa kwa machimbo hayo.

Akizungumza na Shajara, Kamishna wa kaunti ya Marsabit James Kamau amesema kuwa oparesheni ya kuwaondoa wachimba migodi hao inaendelea akisema kuwa kwa sasa utulivu umerejea.

Hii ni kufuatia kisa ambapo mwanaume wa miaka 25 alifariki kutokana na majeraha ya kupigwa mawe baada ya mzozo kuibuka katika machimbo hayo siku ya Jumamosi iliyopita.

Wakati za ziara ya kiusalama katika kaunti ya Marsabit mwezi Mei mwaka 2025, waziri wa Usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen alisema kuwa migodi hiyo 13 itafunguliwa baada ya mikakati yote ya kiusalama kuwekwa ikiwemo ujenzi wa barabara.

Serikali kuu ilipiga marufuku shughuli katika migodi hiyo kufuatia utovu wa usalama japo shughuli katika machimbo hayo zimeripotiwa kuendelea.

Radio Jangwani 106.3FM is a community radio station situated in Marsabit County broadcasting from Marsabit town. It is the brain child of the bishop of catholic diocese of Marsabit, Rt. Rev. Peter Kihara. It is established with the objective of reaching the people Marsabit diocese and Marsabit County for evangelization, Education, entertaining and disseminating information to the masses.

Post Comment